Sunday, December 10, 2017

Watanzania wakerwa na kikosi cha timu ya kilimanjaro stars


 








 
 
 
 
 Wapenda soka wengi nchini wameonekana kukerwa na kikosi cha Kilimanjaro Stars kilichoshiriki michuano ya Chalenji inayoendelea nchini Kenya.

Hata hivyo, kero hiyo imezidi kuwa kubwa baada ya Kocha Mkuu wa Kilimanjaro Stars, Ammi Ninje kusema “always next time”, akimaanisha wakati mwingine baada ya Stars kushindwa kufanya vizuri katika michuano hiyo.

Jana mchana, Stars imefungwa kwa mabao 2-1 na Rwanda ikiwa imetangulia kufunga baadaye Amavubi wakasawazisha na kupata bao la ushindi.

Kili Stars inafungwa mechi ya pili mfululizo baada ya kuwa imelala kwa mabao 2-1 kutoka kwa Zanzibar Heroes ambao walianza kwa kufungwa, wakasawazisha na kupata ushindi.

Wakati akihojiwa, Ninje alionekana ni mchangamfu, akisifia vijana wake walivyocheza na kuongeza kwamba “until next time”.

Mashabiki wa soka wamekuwa wakijadili uwezo wake na baadhi wanaeleza kwamba Uingereza alifundisha timu za watoto na hakuwa na nafasi ya kufundisha timu ya taifa.


Wako ambao wanamtetea ambao ni idadi ndogo na kundi la tatu la mjadala ni lile linalowachambua wachezaji kutoonyesha juhudi.

No comments:

Post a Comment