Beki
kisiki wa kati wa Yanga, Kelvin Yondani anatarajiwa kuikosa mechi ya
kesho dhidi ya ya Ligi Kuu Bara itakayochezwa kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yondani ataikosa mechi hiyo kutokana na kutumikia adhabu ya kadi tatu za njano alizozipata kwenye mechi zilizopita za ligi kuu.
Kutokana
na hali hiyo, timu inaweza kumtumia beki wa kati Nadir Haroub
‘Cannavaro’ au Said Makapu kucheza nafasi hiyo ya beki ya kati pamoja na
Vicent Andrew ‘Dante’.
Taarifa
zinaeleza Benchi la Ufundi la Yanga tayari limeanza kuchukua tahadhari
ya kuwaandaa baadhi ya wachezaji akiwemo Cannavaro atakayecheza nafasi
ya Yondani.
“Yondani
ameondolewa kwenye mipango ya kocha katika kuelekea mechi dhidi ya Ruvu
itakayochezwa Jumapili Uwanja wa Taifa.
“Beki
huyo ataukosa mchezo huo kutokana na kutumikia adhabu ya kadi tatu za
njano alizozipata katika michezo iliyopita ya ligi kuu,” alisema mtoa
taarifa huyo.
Meneja
Mkuu wa Yanga, Hafidh Saleh alithibitisha Yondani kuondolewa kikosini;
“Ni kweli Yondani hatakuwepo katika mechi dhidi ya Ruvu kwani ana adhabu
ya kadi tatu za njano.”
No comments:
Post a Comment