RAIS
wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia ametuma salamu za
rambirambi kufuatia kifo cha beki wa zamani wa kimataifa wa Tanzania,
Omary Kapera aliyefariki dunia juzi kuzikwa jana mchana.
Rais
Karia amesema kwamba amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba
huo; "Nimeshtushwa na taarifa hizo za kifo cha Kapera hasa ikichukuliwa
bado tupo kwenye majonzi ya kumpoteza mchezaji mwingine wa zamani
Athuman Juma Chama, kwa niaba ya Shirikisho natoa pole kwa wote
walioguswa na msiba huo kuanzia kwa familia, ndugu, jamaa na
marafiki,”alisema Rais Karia.
Omar
Kapera ‘Mwamba Kifua’ alikuwa sentahafu wa Yanga tangu miaka ya 1960
hadi 1977 alipokwenda kujiunga na Nyota Afrika ya Morogoro kufuatia
mgogoro mkubwa uliobuka klabu ya Jangwani mwaka 1976.
Kapera
na kundi la wachezaji wenzake walioondoka Yanga baada ya mgogoro huo wa
kihistoria, baadaye walirejea Dar es Salaam kuasisi Pan Africans
iliyokuja kuwa tishio pia katika soka ya Tanzania kabla ya kupoteza
makali baada ya muongo mmoja
Kapera
alikuwepo kwenye kikosi cha Yanga kilichoichapa Simba SC 5-0 Juni 1,
mwaka 1968 Uwanja wa Karume, Dar es Salaam siku hiyo mabao ya wana
Jangwani yakifungwa na Maulid Dilunga mawili dakika ya 18 kwa penalti na
43, Salehe Zimbwe dakika za 54 na 89 na Kitwana Manara ‘Popat’ dakika
ya 86.
Na
ni kikosi hicho kilichofika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika
mara mbili mfululizo mwaka 1969 na 1970 na kutolewa na Asante Kotoko ya
Ghana mara zote
No comments:
Post a Comment