Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma bado ni majeruhi na hajajiunga na wenzake.
Lakini
jana aliamua kuwatembelea wenzake mazoezini kwenye Uwanja wa Uhuru
wakati wakiendelea kujifua kujiandaa na mechi za Ligi Kuu Bara.
Raia
huyo wa Zimbabwe, ameendelea kukaa nje kwa zaidi ya miezi miwili sasa
na imekuwa zaidi ya wiki tatu tokea arejee Dar es Salaam akitokea kwao
Zimbabwe ambako ilielezwa amekwenda kupata matibabu nchini Afrika
Kusini.
No comments:
Post a Comment