Baada ya mgomo wa muda wa takribani wiki mbili, kipa Beno Kakolanya hatimaye amerejea mazoezini Yanga.
Kakolanya
amerejea na kuendelea na mazoezi na wenzake kwenye Uwanja wa Uhuru
jijini Dar es Salaam kuendelea kujiandaa na mechi zijazo za Ligi Kuu
Bara.
Kipa huyo mzoefu aliyejiunga na Yanga akitokea Prisons ya Mbeya, aliweka mgomo akitaka kumaliziwa fedha alizokuwa anadai.
Hata
hivyo, ilionekana uongozi wa Yanga ulikuwa ukipambana kumrejesha Obrey
Chirwa ambaye pia aligomea kwao Zambia kutokana na kutolipwa fedha zake
pia.
Baadaye,
uongozi huo ulifanikiwa kumrekesha Chirwa timu ikiwa kwenye michuano ya
Kombe la Mapinduzi na sasa Kakolanya naye amerejea.
No comments:
Post a Comment