Monday, February 26, 2018

Eden Hazard ni bora zaidi ya Messi na CR7,


Kampuni inayokusanya taarifa za takwimu mbali mbali za michezo iitwayo CIES Football Obsevatory imetoka na taarifa mpya kuhusu kiwango cha wachezaji wenye uwezo mkubwa kwa kukokota mipira(dribles).

STAND UNITED NA PRISONS ZATINGA ROBO FAINALI AZAM SPORTS FEDERATION CUP

TIMU za Tanzania Prisons na Stand United zimekamilisha idadi ya timu nane za kucheza hatua Robo Fainali ya michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi kwenye mechi zao za jana.

WENGER KIBARUA CHAKE CHAINGIA DOSARI

 
KLABU ya Arsenal itaitathmini nafasi ya Arsene Wenger mwishoni mwa msimu — kukiwa na uwezekano wa kuhitimisha miaka 22 ya Mfaransa huyo.

SIMBA YAZIDI KUKWEA KILELENI MWA LIGI VPL

SIMBA SC imezidi kuukimbilia kwa kasi ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Mbao FC ya Mwanza jioni ya jana  Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi alifunga mabao mawili moja kila kwa kipindi kabla ya kuumia na kutolewa wakati mabao mengine yalifungwa na Shiza Kichuya, Erasto Nyoni na Mghana, Nicholaus Gyan.
Ushindi huo unaifanya Simba itimize pointi 45 baada ya kucheza mechi 19, ikiendelea kukaa kileleni mwa Ligi Kuu, ikifuatiwa na mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 37 za mechi 18, wakati Mbao FC inabaki nafasi ya 10 kwa pointi zake 19 za mechi 19.
 li kuanza kupata mabao, benchi la Ufundi la Simba chini ya kocha Mfaransa, Pierre Lechantre anayesaidiwa na Mrundi, Masoud Juma lililazimika kufanya mabadiliko ya mapema kipindi cha kwanza katika safu ya kiungo kwa kumtoa Said Hamisi Ndemla na kumuingiza Muzamil Yassin baada ya nusu saa.
Mabadiliko hayo yalibadilisha kabisa mwelekeo wa mechi, kutoka Mbao FC kutawala hadi Simba SC ambayo wiki ijayo itamenyana na El Masry ya Misri katika Raundi ya Kwanza ya kombe la Shirikisho Afrika kuuteka mchezo.    
Shiza Ramadhani Kichuya akafungua sherehe za mabao za Simba kwa kufunga bao la kwanza dakika ya 38 akimalizia pasi ya mtokea benchi, Muzamil.
Mganda Emmanuel Okwi akaifungia Simba SC bao la pili dakika ya 40 kwa penalti, baada ya yeye mwenyewe kuanguka kwenye boksi wakati anadhibitiwa na beki wa Mbao, David Mwasa.
Refa Erick Onoka kutoka Arusha akawanyima Simba SC penalti sahihi zaidi ya aliyowapa mwanzo baada ya Okwi kuangushwa kwenye boksi na Nahodha wa Mbao FC, Mrundi, Yusuph Ndikumana ambaye leo alicheza chini ya kiwango.
Kipindi cha pili, Mbao FC wanaofundishwa na kocha Mrundi, Etienne Ndayiragijje walikianza vizuri wakishambulia kujaribu kutafuta mabao ya kusawazisha, lakini safu ya ulinzi ya Simba chini ya kipa Aishi Salum Manula ilisimama imara.
Kibao kikaigeukia Mbao FC na wakajikuta wanapachikwa mabao matatu ndani ya dakika 20, Okwi akianza kufunga dakika ya 69 kwa shuti la mguu wa kulia baada ya kupokea pasi ya Muzamil Yassin.
Okwi anatolewa nje anachechemea baada ya kuumia kufuatia kugongana na beki wa Mbao FC, Amos Charles kwenye boksi na nafasi yake kuchukuliwa na Mrundi, Laudit Mavugo.   
Beki mkongwe anayeweza kucheza kama kiungo pia, Erasto Edward Nyoni akaifungia Simba SC bao la nne dakika ya 82 kwa shuti la mpira wa adhabu kutoka umbali wa mita 19 kasoro kidogo, baada ya Muzamil kuangushwa.
Refa Onoka akamtoa nje kwa nyekundu Nahodha wa Mbao FC, Ndikumana dakika ya 84 baada ya kumuonyesha kadi ya pili ya njano kufuatia kumchezea rafu Mavugo Mrundi mwenzake, Mavugo.
Nicholaus Gyan akaifungia Simba SC bao la tano dakika ya 86 kufuatia krosi ya beki wa kulia, Shomary Kapombe kuzua kizaazaa langoni kwa Mbao FC. 
Kikosi cha Simba SC; Aishi Manula, Shomari Kapombe, James Kotei, Yussuph Mlipili, Erasto Nyoni, Asante Kwasi, Jonas Mkude, Said Ndemla, Shiza Kichuya/Rashid Juma dk86, Nicholas Gyan na Emmanuel Okwi/Laudit Mavugo dk80.
Mbao FC; Iyvan Rugumandiye, Boniphace Maganga, Amos Charles, David Mwasa, Yusuph Ndikumana, Ibrahim Njohole/ Said K. Said dk57, Herbet Lukindo, George Sangija, Habibu Hajji, James Msuva/Rajesh Kotecha dk51 na Emmanuel Mvuyekure/Ismail Ally dk70.

YANGA AHUENI MAANDALIZI LIGI YA MABINGWA, YAAHIRISHA MECHI NA MTIBWA

MCHEZO wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya wenyeji Mtibwa Sugar na Yanga SC ya Dar es Salaam uliopangwa kufanyika Machi 3, mwaka huu Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro umeahirishwa. 
Sababu za kuuahirisha mchezo huo namba 170 ni kuipa Yanga nafasi nzuri ya maandalizi ya mchezo wake wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Township Rollers ya Botswana Machi 6 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Busara za Bodi chini ya Mwenyekiti wake, Clement Sanga ambaye pia ni Kaimu Mwenyekiti wa Yanga SC zimeielekeza kuusogeza mbele mchezo wa Ligi Kuu ili kuwapa wawakilishi hao wa Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa fursa nzuri ya maandalizi. 

Baada ya kukata tiketi ya Robo Fainali ya michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) kufuatia ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, Maji Maji Uwanja wa Maji Maji mjini Songea Jumapili, Yanga iliondoka mjini humo mapema Jumatatu kwa basi lake kwenda Mtwara tayari kwa mchezo mwingine wa Ligi Kuu dhidi ya wenyeji, Ndanda FC Jumatano Uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Mabao ya Yanga Jumapili yalifungwa na kiungo Pius Charles Buswita kwa kichwa dakika ya 40 akimalizia krosi ya beki Mwinyi Hajji Mngwali kutoka upande wa kushoto baada ya kuanzishiwa kona fupi na kiungo mwenzake, waliyekuwa wakicheza naye pale mbele, Ibrahim Ajib na winga Emmanuel Martin dakika ya 57 akimalizia kwa kichwa krosi ya beki wa kulia, Hassan Kessy aliyemlamba chenga Mpoki Mwakinyuki.
Bao pekee la Maji Maji lilifungwa na kiungo Jaffar Mohammed kwa kichwa dakika ya 61, akimalizia mpira wa adhabu uliopigwa na beki Aziz Sibo kufuatia Nahodha, Kevin Yondan kumchezea rafu Marcel Boniventura.
Yanga ilikata tiketi ya kwenda Raundi ya Kwanza ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika Jumatano iliyopita licha ya sare ya 1-1 na wenyeji, Saint Louis Suns United katika mchezo wa marudiano wa Raundi ya Awali Uwanja wa Linite.
Mabingwa hao wa Tanzania wamesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 2-1 baada ya Februari 10 kushinda 1-0 pia Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, bao pekee la kiungo Juma Mahadhi aliyekosekana uwanjani kwenye mechi ya marudiano kwa sababu ya homa.
Kwa kuitoa St Louis, Yanga itakutana na Township Rollers ya Botswana katika Raundi ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika, ambayo nayo iliitoa El Merreikh ya Sudan, mechi ya kwanza ikichezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Machi 6 kabla ya kwenda Gaborone kwa mchezo wa marudiano, Machi 17.

Saturday, January 27, 2018

Real madrid yaicha 4-1 valencia


Cristiano Ronaldo (kulia) akishangilia na wenzake kumpongeza Marcelo baada ya kuifungia Real Madrid bao la tatu dakika ya 84 katika ushindi wa 4-1 dhidi ya wenyeji, Valencia kwenye mchezo wa La Liga leo Uwanja wa Mestalla. Ronaldo naye alifunga mabao mawili, yote kwa penalti dakika za 16 na 38 wakati bao la nne limefungwa na Toni Kroos dakika ya 89, huku la Valencia likifungwa na Santi Mina dakika ya 58

Morocco na Sudan zatinga nusu fainali CHAN



WENYEJI, Morocco na Sudan wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali za michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) baada ya ushindi dhidi ya Namibia na Zambia usiku wa jana.

SIMBA KUTANDAZA SOKA SAFI MBELE YA MFARANSA LEO

 Image result for kikosi cha simba picha 
RAUNDI ya kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inahitimishwa leo kwa michezo miwili, vinara Simba SC wakiwakaribisha Maji Maji ya Songea

Saturday, January 20, 2018

Uganda yatupwa nje CHAN


 TIMU ya Taifa ya Uganda imetolewa kwenye michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN),

safari ya Ndemla ziiiiiii


KIUNGO wa Simba, Said Ndemla, sasa anajiandaa kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuwepo Msimbazi huku ikielezwa lile dili la kwenda kucheza Ulaya limeyeyuka.
Ndemla ambaye mkataba wake wa sasa na Simba unamalizika Aprili, mwaka huu, mwishoni mwa mwaka jana alikwenda Sweden kufanya majaribio kwenye timu ya AFC Eskelistuna na kufuzu.

Hata hivyo, licha ya kufuzu majaribio hayo, Ndemla ameshindwa kujiunga na timu hiyo.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa, uongozi umeridhishwa na kiwango cha Ndemla, hivyo wameona bora waendelee kuwa naye ili kukiongezea nguvu kikosi katika mechi za Kombe la Shirikisho Afrika.

“Mkataba wake unaelekea ukingoni lakini wakati wowote anaweza kuongezewa kwa sababu uongozi unaridhishwa na kiwango chake ukizingatia kwamba tuna michuano ya kimataifa.
“Hii inamaanisha kuwa, huu si wakati wa kuacha wachezaji kama yeye,” kilisema chanzo hicho.

Alipotafutwa meneja wa mchezaji huyo, Jamal Kisongo kuzungumzia mustakabali wa Ndemla, alisema: “Lile dili lake kule Sweden tumewaachia Simba waamue kwani bado ni mchezaji wao, vyovyote watakavyosema ni sawa hakuna shida.”

Wakati hayo yakijiri, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amemuahidi kiungo huyo kumpatia gari kutokana na kiwango chake bora alichokionyesha msimu huu

Ujio wa Pierre-Emerick Aubameyang Arsenal ni dawa


Straika Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Borussia Dortmund ya Ujerumani.
LONDON, England
ARSENAL chini ya kocha wake Arsene Wenger inapambana kuhakikisha inamsajili straika Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Borussia Dortmund ya Ujerumani.
Aubameyang raia wa Gabon anatakiwa na Arsenal kwa udi na uvumba ili kuziba nafasi ya straika Alexis Sanchez ambaye anatarajiwa kujiunga na Manchester United au Manchester City.
Maisha ya Aubameyang katika Klabu ya Borussia Dortmund sasa siyo mazuri na inaonekana wazi straika huyo anataka kuondoka na klabu iliyoonyesha nia ya kumsajili ni Arsenal.
Wenger hana jinsi zaidi ya kumuachia Sanchez kwenda jijini Manchester kwani isipofanya hivyo sasa, inaweza kumtoa bure katika usajili ujao kabla ya msimu mpya.
Hata hivyo zipo sababu zinazoonyesha kuwa, Aubameyang anaweza kuisumbua Arsenal kutokana na sababu zifuatazo:
#5 Kulazimisha ushindi
Aubameyang anajua kufunga na akiwa karibu na lango ni mtu hatari sana kwa wapinzani. Hata hivyo, ana tatizo la kutokuwa mpambanaji kwa ajili ya timu na hana njia nyingi za kuwabuguzi mabeki, akishindwa njia moja ndiyo basi tena. Anategemea kufunga kwa kutengenezewa nafasi na wakishindwa kumfanyia hivyo ndiyo basi tena.

#4 Tatizo la ulinzi
Moja kati ya matatizo makubwa ya Aubameyang awapo uwanjani ni mchango wake wa kukaba. Kwa soka la sasa hasa England, kukaba ni kazi ya mshambuliaji pia ili kupunguza kasi ya adui. Sasa Aubameyang yeye si mzuri katika kukaba hivyo atapata tabu katika mfumo huo.

#3 Hayupo kama zamani
Aubameyang wa sasa si yule wa msimu mmoja au miwili nyuma, ameshuka pia vituko vyake nje ya uwanja ni tatizo kichwani mwake. Sawa, sasa anaweza kuwa amefunga mabao 21 katika mechi 23 msimu huu, lakini hailingani na nafasi anazopoteza uwanjani sasa katika kikosi cha Borussia Dortmund.
#2 Gharama yake haiendani na umri
Aubameyang sasa ana umri wa miaka 28, hivyo dau la Borussia Dortmund la kumuuza kwa pauni milioni 53 (Sh bilioni 162.8), haiwezi kuwa na faida kwao kwani hatoweza kucheza kwa ushindani kwa muda mrefu. Hii ina maana kuwa, Arsenal haitaweza kumtumia kwa muda mrefu.

#1 Hawezi kuwa Alexis Sanchez
Ukweli ni kwamba, Aubameyang hawezi kuwa mbadala sahihi wa Alexis Sanchez. Arsenal inadhani Aubameyang ndiye mbadala sahihi wa Sanchez lakini ukweli ni kwamba wawili hao wapo tofauti kabisa. Aubameyang anacheza kwa mtindo mmoja na kwa kutumia upande mmoja tu lakini Sanchez yupo pande zote. Hapa ndipo Arsenal inapoongeza nguvu pia kumnasa Malcom wa Bordeaux.

Beno Kakolanya hatimaye amerejea mazoezini Yanga.


Baada ya mgomo wa muda wa takribani wiki mbili, kipa Beno Kakolanya hatimaye amerejea mazoezini Yanga.

Kakolanya amerejea na kuendelea na mazoezi na wenzake kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kuendelea kujiandaa na mechi zijazo za Ligi Kuu Bara.

Kipa huyo mzoefu aliyejiunga na Yanga akitokea Prisons ya Mbeya, aliweka mgomo akitaka kumaliziwa fedha alizokuwa anadai.

Hata hivyo, ilionekana uongozi wa Yanga ulikuwa ukipambana kumrejesha Obrey Chirwa ambaye pia aligomea kwao Zambia kutokana na kutolipwa fedha zake pia.


Baadaye, uongozi huo ulifanikiwa kumrekesha Chirwa timu ikiwa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi na sasa Kakolanya naye amerejea.

ngoma awatembelea wachezaji wenzake mazoezini

Mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma bado ni majeruhi na hajajiunga na wenzake.

Lakini jana aliamua kuwatembelea wenzake mazoezini kwenye Uwanja wa Uhuru wakati wakiendelea kujifua kujiandaa na mechi za Ligi Kuu Bara.

Raia huyo wa Zimbabwe, ameendelea kukaa nje kwa zaidi ya miezi miwili sasa na imekuwa zaidi ya wiki tatu tokea arejee Dar es Salaam akitokea kwao Zimbabwe ambako ilielezwa amekwenda kupata matibabu nchini Afrika Kusini.
 

Beki kisiki wa kati wa Yanga,nje dhidi ya Ruvu Shooting

Beki kisiki wa kati wa Yanga, Kelvin Yondani anatarajiwa kuikosa mechi ya kesho dhidi ya  ya Ligi Kuu Bara itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Yondani ataikosa mechi hiyo kutokana na kutumikia adhabu ya kadi tatu za njano alizozipata kwenye mechi zilizopita za ligi kuu.

Kutokana na hali hiyo, timu inaweza kumtumia beki wa kati Nadir Haroub ‘Cannavaro’ au Said Makapu kucheza nafasi hiyo ya beki ya kati pamoja na Vicent Andrew ‘Dante’.

Taarifa zinaeleza Benchi la Ufundi la Yanga tayari limeanza kuchukua tahadhari ya kuwaandaa baadhi ya wachezaji akiwemo Cannavaro atakayecheza nafasi ya Yondani.

“Yondani ameondolewa kwenye mipango ya kocha katika kuelekea mechi dhidi ya Ruvu itakayochezwa Jumapili Uwanja wa Taifa.

“Beki huyo ataukosa mchezo huo kutokana na kutumikia adhabu ya kadi tatu za njano alizozipata katika michezo iliyopita ya ligi kuu,” alisema mtoa taarifa huyo.


Meneja Mkuu wa Yanga, Hafidh Saleh alithibitisha Yondani kuondolewa kikosini; “Ni kweli Yondani hatakuwepo katika mechi dhidi ya Ruvu kwani ana adhabu ya kadi tatu za njano.”

sababu za beki mpya wa Yanga kutokuonekana uwanjani

BEKI mpya wa Yanga, Mkongo Fiston 'Festo' Kayembe Kanku ameshindwa kujiunga na timu tangu asajiliwe Desemba kutokana na matatizo ya kifamilia.

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo awatembelea serengeti boys

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe leo amewatembelea wachezaji wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys waliopo kambini kwenye hostel za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), zilizopo Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Katika ziara yake hiyo, Waziri Mwakyembe alijionea namna wachezaji hao wanaoshi na kufanya mazoezi chini ya walimu wao, Mdenmark Kim Poulsen na Msaidizi wake, Oscar Milambo.
Pamoja na kuzungumza nao na kuwatia moyo ili wajitume zaidi, Waziri Mwakyembe aliwaachia ujumbe wa Serikali wachezaji wa Serengeti Boys ambao wote hawazidi umri wa miaka 16.
Dk. Mwakyembe akitoa salamu za Serikali amewaambia vijana wanaounda timu hiyo kuwa serikali yao inawaamini na wanalo jukumu la kuiperusha vyema bendera ya Tanzania. 
Amewataka kupambana kwaajili ya Tanzania na kuhakikisha wanafanya vyema kwenye kila mashindano huku akiwataka makocha wa kikosi hicho kuwapa mafunzo mazuri kwa ustawi wa Vijana hao. 
Aidha, Dk. Mwakyembe amesema anaamini Vijana hao watakuwa bora chini ya TFF iliyopo madarakani inayoongozwa na Rais Ndugu Wallace Karia. 
"Naamini mtaimarika na kuwa bora maana hata TFF hii sasa ina ari na morali kubwa" amesema Dk. Mwakyembe. 
Katika ziara yake hiyo Dk. Mwakyembe alipata nafasi ya kutazama Serengeti Boys ikiifunga 4-1 Makongo Sekondari katika mchezo wa kirafiki.
Kabla ya mchezo huo Serengeti Boys walicheza mchezo mwingine wa kirafiki dhidi ya Kituo cha Bombom na kutoa sare ya kufungana bao 1-1.
Wachezaji 34 wakiwemo 30 wa ndani na makipa wane, wapo kambini Serengeti Boys tangu mwanzoni mwa mwezi hadi Januari 28, 2018 kwa maandalizi ya michuano CECAFA Challenge U-17. 
Maandalizi hayo ya Serengeti Boys yatakwenda sambamba na kucheza mechi za kirafiki kabla ya kuhairisha kambi hiyo itakayokuwa ikifanyika mara kwa mara na mpango uliopo ni kila mwezi timu hiyo kuingia kambini.

Sunday, January 14, 2018

AZAM WAMPA KIUNGO WAO ZAWADI YA UBINGWA


Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Azam Fc imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi, hiyo ni baada ya kuifunga URA ya Uganda kwa penati 4-3.
Awali katika dakika 90 za mchezo huo, timu hizozilitoka suluhu ya 0-0 katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Amaan, jana usiku kisiwani Unguja.

Baada ya kukabidhiwa ubingwa huo, taarifa kutoka Azam FC zinaeleza kuwa ubingwa huo wameutoa zawadi kwa kiungo wa timu hiyo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, na hii ni baada ya kufiwa na Mama yake mzazi wiki iliyopita wakati akiwa na timu hiyo kwenye harakati za kuwania taji hilo.
Hadi Azam FC inatwaa ubingwa, imeweza kucheza jumla ya mechi sita, ikishinda mara tano na kupoteza mmoja huku ikiruhusu nyavu zake kuguswa mara moja tu, na hii ni walipofungwa bao 1-0 dhidi ya URA kabla ya kulipa kisasi kwenye mchezo huo wa fainali.
Kikosi hicho kilitarajiwa kuondoka visiwani Zanzibar, asubuhi ya leo Jumapili kurejea jijini Dar es Salaam tayari kabisa kuanza maandalizi ya kuwakabili Majimaji ya Songea na Tanzania Prisons ya Mbeya, katika mechi zijazo mbili za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) zitakazofanyika wiki ijayo.

JOSE MOURINHO AMPA MANENO MATAMU SANCHEZ


Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho.
KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho amethibitsha kwa ujanja kuwa naye anamtaka Alexis Sanchez baada ya kumpa sifa nyingi.
Mourinho alisema ni vigumu kwa klabu yoyote kuacha fursa ya kusajili nyota mwenye kipaji aina ya Sanchez akitokea yupo soko.

Alexis Sanchez.
“Klabu yoyote makini iwe kama ni Januari, Februari au Julai ikitokea kuna staa yupo sokoni lazima itamchangamkia ingawa sina maana ya Sanchez,” aliongea kijanja Mourinho.

Mourinho alidai hataki kuongelea zaidi kuhusu Sanchez ingawa anamkubali kama mchezaji mzuri mwenye kipaji cha hali ya juu.

Manchester City na Manchester United ziko kwenye vita kali ya kumwania Sanchez, ambaye mkataba wake na Arsenal unamalizika mwishoni mwa msimu huu.

Manchester United inadaiwa imetenga dau la kiasi cha pauni milioni 35 na iko tayari kumpa mshahara wa pauni 250,000 kwa wiki.

Wednesday, January 10, 2018

Imani za kishirikina za mtesa Romelu Lukaku


Mapya yameibuka baada ya moja kati ya matajiri wa klabu ya Everton Farhadi Moshri kuibuka na kutaja masuala ya ushirikina kuwa kati ya mambo ambayo yalimfanya Lukaku kuondoka katika klabu yao.

Usajili wa Coutinho waiumiza United


Ni mwendo wa pesa tu barani Ulaya, na kwa sasa kila mchezaji maarufu ukimgusa lazima uwe na kuanzia £70m na ndio maana haikushangaza sana kwa Philippe Coutinho kwenda Barcelona kwa dau la £145m.

Simba SC Hawawezi Kuwa Ubingwa,Rage


Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage, ameibuka na kusema kuwa, ndani ya klabu hiyo kuna tatizo na kama hawa­takuwa makini, basi kuna uwezekano hata ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu timu hiyo ikauokosa.

KWASI APIGWA BITI KALI


BENCHI la ufundi la Simba chini ya kaimu kocha wake mkuu, Masoud Djuma, raia wa Burundi, limempa tahadhari beki mpya wa timu hiyo, Asante Kwasi, raia wa Ghana,

CHIRWA APELEKA KILIO JANGWANI


Ikiwa ndiyo siku ya kwanza anaichezea Yanga katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, mshambuliaji Obrey Chirwa amekosa penalti ya mwisho na kuing’oa Yanga katika michuano ya Mapinduzi.

TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MSIBA WA KAPERA

RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha beki wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Omary Kapera aliyefariki dunia juzi kuzikwa jana mchana.

YANGA FC YAMFUATA MTANI DAR BAADA YA KUONDOSHWA KWA MIKWAJU YA PENATI 5-4

YANGA SC itapanda boti kurejea mjini Dar es Salaam kesho baada ya kutolewa kwenye michuano ya Kombe la Mapunduzi kwa penalti 5-4 na URA ya Uganda

Saturday, January 6, 2018

CHIRWA ATUA DAR KIMYA KIMYA


MZAMBIA wa Yanga, Obrey Chirwa, amerejea nchini juzi Ijumaa usiku akitokea kwao, huku uongozi ukisisitiza kwamba kuna ishu wanaweka sawa kabla hajajiunga na wenzie Zanzibar.

Okwi na Niyonzima Kumbe Lao Moja

EMMANUEL Okwi amewaambia mashabiki wa Simba kwamba licha ya yeye kutokuwa sehemu ya kikosi kwa sasa katika michuano ya Mapinduzi lakini kwa jinsi alivyoona kwenye Azam TV hakuna ya kuwazuia kubeba ndoo.

COUTINHO ASAINI MIAKA MITANO NA NUSU BARCELONA

Mbrazil Philippe Coutinho amesaini mkataba wa miaka mitano na nusu kujiunga na Barcelona


Takwimu za Coutinho Liverpool 

2012-13 Mechi 13, mabao 3
2013-14 Mechi 37, mabao 5
2014-15 Mechi 52, mabao 8
2015-16 Mechi 43, mabao 12
2016-17 Mechi 36, mabao 14
2017-18 Mechi 18, mabao 12 
HATIMAYE Philippe Coutinho ni mchezaji mpya wa Barcelona ya Hispania baada ya uhamisho wa Pauni Milioni 145 kutoka Liverpool.  
Picha zilimuonyesha kiungo huyo Mbrazil akisafiri

SAMATTA AANZA MAZOEZI MAALUM

NAHODHA wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ameanza mazoezi mepesi chini ya uangalizi wa Daktari baada ya kupona maumivu ya goti yaliyomuweka nje kwa miezi miwili. 

Friday, January 5, 2018

maneno kati ya Jose Mourinho na Antonio Conte yafikia pabaya


Jose Mourinho na Antonio Conte kwa muda sasa wamekuwa wakitupiana maneno ya chinichini katika mikutano na waandishi wa habari japo chanzo haswa cha wawili hao kurushiana vijembe hakifahamiki.

Nyota wa Tanzania kujenga kituo cha soka

Beki wa Tanzania anayekipiga kwenye klabu ya Baroka FC inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini Afrika Kusini, Abdi Banda amesema mwaka huu ana mpango wa kufungua kituo cha kukuza vipaji vya soka mkoani Tanga.


"Malengo yangu ni kuwasaidia vijana wenzangu wa Kitanzania na mwaka huu natarajia kufungua kituo cha kukuza vipaji jijini Tanga," amesema Banda.
Banda amesema atafanya hivyo kwasababu anatambua kuwa wapo vijana wengi ambao wana ndoto za kufika mbali zaidi kisoka, hivyo wanahitaji msaada kutoka kwa watu ambao wapo mbele katika soka.
''Unapocheza nje ya Tanzania ni vizuri kuonyesha mchango wako kwa vijana walio chini yako, kwahiyo hilo ndio lengo langu na sitaishia tu kujenga kituo nitaendelea kutoa vifaa vya michezo kwaajili ya vijana wenye ndoto za kuwa wachezaji wakubwa'', ameongeza.

Banda alisajiliwa na Baroka FC kwenye usajili wa kiangazi Juni 2017, baada ya kuonesha kiwango kizuri alipokuwa nchini Afrika Kusini na kikosi cha Taifa Stars kwenye michuano ya COSAFA 2017. Baroka inashika nafasi ya nne kwenye ligi kuu ya humo ikiwa na alama 22 baada ya michezo15

Yanga watoa fursa kwa vijana wenye vipaji

Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara Yanga SC, imetangaza fursa kwa vijana wenye vipaji vya soka kufanya usaili kwaajili ya kusajiliwa na timu hiyo.

kocha wa Azam akoshwa na mshambuliaji Arthur


Bosi wa benchi la ufundi la Azam FC, Aristica Cioaba, raia wa Romania na wasaidizi wake, wanakoshwa na soka la mshambuliaji wao mpya, Bernard Arthur raia wa Ghana ambaye amekuwa msaada mkubwa katika ushambuliaji. 

Cannavaro: Yanga inaweza kuchukua ubingwa wa mapinduzi

Kapteni wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amewapoza mashabiki wa timu yake kwa kuwaambia watulie kwani wao wachezaji wamejipanga kutwaa ubingwa wa Kombe la Mapinduzi mwaka huu.

LUKAKU ,LINGARD WAINGIA NYAVUNI WAIUA DERBY 2-0 FA CUP


MANCHESTER UNITED: (4-2-3-1) Romero 6; Lindelof 6, Smalling 7, Blind 6, Shaw 6.5; Herrera 6, Pogba 7; Mata 6 (Martial 67, 6.5), Lingard 7.5, Mkhitaryan 5 (Lukaku 46, 5.5); Rashford 5 (Fellaini 80)
SUBS NOT USED: Rojo, Darmian, McTominay, Pereira 
GOALS: Jesse Lingard (84)
COACH: Jose Mourinho


DERBY: (4-2-3-1) Carson 7; Wisdom 6.5, Keogh 7, Pearce 6, Olsson 6.5; Thorne 6, Huddlestone 6.5; Russell 6.5 (Hanson 78, 6), Lawrence 6.5 (Bennett 81), Weimann 6; Winnall 6 (Vydra 67, 6)
SUBS NOT USED: Mitchell, Baird, Martin, Nugent
COACH: Gary Rowett
REFEREE: Kevin Friend 7
MAN OF THE MATCH: Jesse Lingard
VENUE: Old Trafford
ATTENDANCE: 73,899

Mesen Seleta Ampa Wakati Mgumu Pam D





Pam D na Mesen Selekta.
MSANII wa Bongo Fleva, Pamela Daffa ‘Pam D’ amejikuta kwenye wakati mgumu wa kumfariji ndugu yake ambaye pia ni msanii mwenzake, Mesen Selekta kutokana na kufiwa na mama yake ambaye alimfia mikononi mwake.

Nitawafunga Mpaka Mkome


Kaimu Kocha wa Simba, Masoud Djuma, akiamini Asante Kwasi atawasaidia kutwaa mataji msimu huu, beki huyo amepania kufanya mambo makubwa zaidi hasa kufunga mabao muhimu.

JKT RUVU YAJA KIVINGINE, SASA YAITWA JKT TANZANIA

TIMU ya JKT Ruvu inayoshiriki Ligi Daraja La Kwanza Tanzania Bara Kundi A msimu huu, sasa itajulikana kwa jina la JKT Tanzania SC.