Sunday, November 5, 2017

City waendelea kuweka rekodi mpya

Mchezo wa pili kati ya michezo kumi iliyopita Pep Gurdiola anapata ushindi zidi ya Arsenal ushindi ambao unawafanya Manchester City kuendelea kutawala katika ligi ya Epl.


Alikuwa Kelvin De Bruyne dakika ya 19 ndio alizifungua nyavu za Arsenal baada ya kupiga shuti lililomshinda mlinga lango wa Arsenal Petr Cech.
Goli la leo la Kelvin De Bruyne zidi ya Arsenal linamfanya kuifunga Arsenal bao mbili na kutoa assist mbili katika michezo 5 ambayo Mbelgiji huyo amecheza zidi ya Arsenal.
Ushindi wa leo wa City ni muendelezo wa rekodi mbovu ya Arsenal ambao hawajawahi kushinda mchezo wowote Epl wa ugenini ambao walimaliza kipindi cha kwanza wakiwa wamefungwa ndani ya miaka 6.
Kun Aguero aliifungia Manchester City bao la pili kwa mkwaju wa penati bao ambalo linawafanya Arsenal kuwa timu inayoongozwa kwa kufungwa magoli ya penati tangia kuanza kwa msimu uliopita.
Lakini Alexandre Lacazette aliyeingia akitokea benchi aliipatia Arsenal bao la kufutia machozi dakika ya 65 na kuwafanya Arsenal kuwa timu ambayo yenye mabao mengi kutoka kwa wachezaji wa akiba kuliko timu yoyote Epl tangu msimu uliopita (mabao 13).
Dakika ya 74 Manchester City walifunga bao ambalo lilizua utata kutoka kwa Gabriel Jesus baada ya kuonekana kama wachezaji wa City walikuwa offside na mchezo kumalizika kwa City kushinda 3 kwa 1.
Mabao matatu waliyopata Manchester City hii leo yanawafanya kufikisha idadi ya mabao 57 katika mechi zao 17 msimu huu idadi ambayo mara ya mwisho kutokea Epl ilikuwa msimu wa mwaka 1992/1993.

No comments:

Post a Comment