Mbegu
hizo zimepokelewa na wakulima chini ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri
ya Wilaya ya Mbogwe Nsika Sizya ambaye amesema kuwa mbegu hizo
zitaongeza chachu ya kilimo wilayani humo.
“Changamoto kubwa waliyokuwa nayo
wakulima katika Halmshauri yetu ni kukosekana kwa mbegu bora za mihogo
na mahindi ila baada ya kupata mbegu hizi zitaongeza ari na chachu ya
kilimo kwa wananchi”, amesema Sizya.
Mbali na mbegu ya mahindi lakini pia Tume ya Taifa ya Sayansi na
Teknolojia imekabidhi mbegu ya mihogo aina ya Mkombozi ambayo inauwezo
mkubwa wa kustahimili magonjwa ya mihogo kama batobato na michirizi ya
kahawia ambayo imekuwa ikiwapatia hasara kubwa wakulima wengi na
kupoteza hadi asilimia 90 za mazao.
Mbegu hiyo itanufaisha wakulima wa vijiji vinne vya Mponda kilichopo
Kata ya Luganga, kijiji cha Ushetu kilichopo Kata ya Ushirika, kijiji
cha Lwazeze kilichopo Kata ya Ngemo na kijiji cha Iponya kilichopo Kata
ya Iponya.
No comments:
Post a Comment