Timu ya taifa ya Ubelgiji ilikuwa uwanjani usiku wa jana kukabiliana na
timu ya taifa ya Mexico ambapo katika mchezo huo Romelu Lukaku alifunga
mabao mawili kati ya matatu katika suluhu ya tatu tatu.
Eden Hazard alifunga lingine huku mabao ya Mexico yakipatikana
kupitia kwa Andres Guardado aliyefunga kwa penati kabla ya Hirving
Lozano kuongeza mengine mawili.
Ufaransa wenyewe walikuwa uwanjani na timu yao inayosadikiwa kuwa ni
kizazi cha dhahabu na kuwafunga Wales 2 kwa nunge kupitia kwa Antoine
Griezman na Olivier Guroud.
Timu
ya taifa ya Ureno nao bila Cr7 walicheza na Saudi Arabia ambapo Ureno
waliibuka kidedea kwa mabao 3 kwa nunge mabao ya Ureno yakifungwa na
Fernandes, Guedes pamoja na lile la Mario.
Katika hatua ya mtoano kuelekea kombe la dunia timu ya taifa ya Sweden
iliishtua Italia baada ya kuwafunga bao 1 kwa nunge na hivyo kuwaweka
Italia mashakani kulekea kombe la dunia 2018.
No comments:
Post a Comment