Saturday, October 28, 2017

RATIBA MECHI ZA WEEK END HII

RATIBA ZA MECHI WEEK END HII  Saturday 28 October

Manchester United 13:30 Tottenham

Arsenal 16:00 Swansea

Crystal Palace 16:00 West Ham

Liverpool 16:00 Huddersfield

Watford 16:00 Stoke

West Bromwich 16:00 Manchester City

Bournemouth 18:30 Chelsea                             
Sunday 29 October

Brighton 14:30 Southampton

Leicester 17:00 Everton
Monday 30 October

Burnley 21:00 Newcastle

   LALIGA 
Saturday 28 October

Alaves 13:00 Valencia

Atletico Madrid 18:30 Villarreal

Athletic Bilbao 20:45 Barcelona

Sevilla 22:30 Leganes
Sunday 29 October

Getafe 12:00 Real Sociedad

Girona 16:15 Real Madrid

Eibar 18:30 Levante

Malaga 20:45 Celta Vigo
Monday 30 October

Espanyol 21:00 Betis

Las Palmas 21:00 Deportivo La Coruña
 
                                                                                                            

KAMPENI YA ‘KIWANDA CHANGU, MKOA WANGU’ KUANZA MIKOANI

jafo pics

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo.
………………………………………………………………
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Mhe. Selemani Jafo ameagiza mikoa yote kuanza Kampeni kabambe iitwayo ‘Kiwanda changu Mkoa wangu’ ili kuharakisha maendeleo na kuongeza upatikanaji wa ajira kwenye maeneo hayo.
Jafo ametoa maagizo hayo ya wizara yake kwa Wakuu wa mikoa yote ya Tanzania bara wakati alipokuwa akizungumza na Wakuu wa mikoa sita wapya walioapishwa leo na Rais Dk.John Magufuli.
Akizungumza na Wakuu hao baada ya kukamilisha kwa zoezi la kiapo, Jafo amesema kampeni hiyo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwezi Desemba mwaka huu.
Amesema Mpango huo kabambe ni wa kuhamasisha ujenzi wa viwanda vidogo na vya kati katika mamlaka za serikali za mitaa.
“Hii sasa ni changamoto kwenu wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya hapa nchini nataka kila mkoa ujenge angalau viwanda 100 kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Desemba 2017 hadi Desemba 2018,”anasema jafo
Amebainisha malengo yake ni kwamba ndani ya kipindi hicho cha mwaka mmoja zaidi ya viwanda vidogo na vya kati 2600 viwe vimejengwa nchini.
Katika kufanikisha mpango huo, Waziri Jafo amewataka maafisa wa maendeleo ya jamii kufanya kazi ya kuviunganisha vikundi vilivyopo katika halmashauri zao ili viweze kupata fursa za mifuko mbalimbali ya uwezeshaji iliyo chini ya Ofisi ya Waziri mkuu na fedha za uwezeshaji vijana na wanawake katika halmashauri zao.
Kampeni hiyo endapo itafanikiwa basi itakuwa ni mchango mkubwa kutoka wizara ya TAMISEMI katika ajenda ya viwanda hapa nchini.

ACHOMA NYAVU KUKOMESHA UVUVI HARAMU.........WAZIRI MPINA

DSC_0007

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akimimina mafuta ya taa kabla ya zoezi la kuteketeza nyavu zinazotumika katika uvuvi haramu mjini Kigoma leo. Nyuma yake ni baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Kigoma watumishi wa umma na wanahabari wakishuhudia tukio hilo.

 DSC_0009
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akiwasha moto kuteketeza nyavu zinazotumika katika uvuvi haramu Mjini Kigoma leo.

DSC_0010 

Nyavu zinazotumika katika uvuvi haramu zenye dhamani ya shilingi milioni 31 zikiteketea kwa moto kuashiria kuanza rasmi kwa zoezi la kupambana na uvuvi haramu nchini.

Waziri wa Mifugo na uvuvi Luhaga Mpina ameteketeza nyavu zinazotumika katika uvuvi haramu zilizokamatwa mkoani Kigoma zenye thamani ya shilingi Milioni thelalini na moja kuashiria kuanza rasmi kwa zoezi hilo katika serikali hii ya awamu ya tano.
Akiongea mara baada ya kuteketeza nyavu hizo hizo mapema leo, Mpina alionyesha kushangazwa na suala la uvuvi haramu kuwa sugu “kwa nini vita hii haina mwisho? Lazima yawezekana mbinu zinazotumika ni dhaifu ama silaha zinazotumika ni duni, ifike mahala suala hili  liwe historia”. Alisema Mpina.
Akitoa Maelekezo kwa viongozi wa Mikoa ambayo shughuli hizi zinafanyika, Mpina aliwataka viongozi hao wawe na jukumu la kulinda rasilimali za taifa ikiwa ni mapoja na Bahari, Maziwa na mito.
“kama nitashindwa kushughulia suala zima la uvuvi haramu, niitaaachia dhamana hii niliyopewa na Mheshimiwa Rais, na mpaka kufikia hatua hiyo lazima wengi watakuwa wamejuruhiwa.” Alisisitiza Mpina.
Akiwa katika ziara ya Oparesheni Maalum ya Ondoa Mifugo kutoka katika mikoa ya mipakani na nchi jirani akiwemo Mkoani kigoma, Mpina Pia alitembea mwalo mpya wa Kibirizi Mjini Kigoma na kumtaka Afisa Mifugo na Uvuvi na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma kushughulikia changamoto za mitambo wa kugandisha barafu inayokikabili kikundi shirikishi cha rasilimali za uvuvi mwaloni hapo pamoja na suala la kuwauzia dagaa wafanya biashara wanaozisafirisha nje ya nchi. Waziri Mpina Pia alitembelea chuo uvuvi mjini Kigoma.
Zoezi la opareshini ondoa mifugo na kukomesha rasmi uvuvi haramu limeanza rasmi kwa viongozi wa Wizara husika wakiongozwa na mawaziri Luhaga Mpina na Abdalah Ulega kuingia kazini katika mikoa inayokabiliwa na changamoto hizo.
 

HABARI ZILIZOPEWA KIPAUMBELE KATIKA MAGAZETE YA LEO 28 OCTOBER 2017