NINI CHANZO
NA ASILI YA UCHAWI KATIKA KISIWA CHA UKEREWE ?...
Kwa mujibu wa
utafiti, mpaka mwaka 1500, kisiwa cha Ukerewe hakikuwa kinakaliwa na watu.
Yaani kwa lugha ya kitaalamu zaidi , tunaweza kusema, kisiwa cha Ukerewe
kilikuwa TERRA NULIUS. Hakukuwa na mtu yoyote aliyekuwa anaishi kwenye kisiwa
cha Ukerewe zaidi ya kuwa pori kubwa linalo kaliwa na wanyama wa mwituni.
Wavuvi wachache kutoka katika maeneo ya Mwanza, Sengerema( Uvinza), Kagera na
Mara walikuwa wanapita katika kisiwa hicho katika shughuli zao za uvuvi
WATU WALIANZA VIPI KUISHI UKEREWE
Rekodi zinaonyesha kuwa, kisiwa cha Ukerewe kimeanza
kukaliwa na watu mwishoni mwa miaka ya 1700 au mwanzoni mwa miaka ya 1800.
katika kipindi chote ambacho kisiwa cha Ukerewe hakikuwa kinakaliwa na watu,
wachawi kutoka Gamboshi na maeneo mbalimbali ya kanda ya ziwa kama vile Mwanza,
Shinyanga, na mikoa ya Tabora, Singida na Kigoma, walikuwa wanakitumia kisiwa
cha ukerewe kama himaya ya kufanya shughuli zao za kichawi.
Wachawi hawa hawakuwa wakiishi katika kisiwa hicho,
bali waliishi katika maeneo mbalimbali ya kanda ya ziwa, ila kisiwa cha ukerewe
walikitumia kwa ajili ya kufanya shughuli zao mbalimbali za kichawi kama vile
kufuga misukule. Kufanya ibada za kichawi, kuwalimisha watu kichawi, kufanya
kafara za kichawi nakadhalika.
Watu wa kwanza kwenda kuishi katika kisiwa cha
ukerewe walikuwa ni wavuvi wakifuatiwa na wakulima kisha wafanyabiashara kutoka
katika maeneo ya Mwanza, Sengerema, Majita na Bukoba. Hii kwa lugha nyingine ni
sawa na kusema kuwa kisiwa cha ukerewe kilianzishwa na wavuvi na wakulima
kutoka katika mikoa ya Mwanza, Kagera & Mara.
Nadharia hii inasema kuwa watu wa kwanza kufika
katika kisiwa cha Ukerewe walikuwa ni wavuvi kutoka katika mkoa wa Mwanza.
Wavuvi hawa walifika katika kisiwa cha Ukerewe wakiwa katika harakati zao za
kutafuta eneo lenye samaki wengi.
Inasemekana kuwa , wavuvi hawa walifurahishwa sana
na uwingi wa samaki waliokuwa wanapatikana katika kisiwa cha Ukerewe, ambapo
waliamu kupiga kambi yao kabisa katika kisiwa hicho na biashara yao ikawa ni
kuwatoa samaki Ukerewe na kuwapeleka Mwanza, Mara na Bukoba.
Baadaye wavuvi wengine pamoja na wafanyabiashara wa
samaki kutoka Mwanza , Mara na Kagera nao waliamua kwenda kuweka makazi yao
katika kisiwa hicho baada ya kupata sifa zake nzuri.. Kutokana na ardhi yake
kuwa nzuri na yenye rutuba, wakulima kutoka katika mkoa wa Mwanza walianza
kufanya shughuli za kilimo katika kisiwa hicho, wakijikita zaidi katika mazao
ya nyanya, mbogamboga kama vile mchicha, pamoja na machungwa kwa kutaja
vichache.
Sifa nzuri za kisiwa cha ukerewe ziliendelea
kusambaa na kuzidi kuwavutia wana kanda ya ziwa ambapo sasa wakaanza kumiminika
kwa wingi wao katika kisiwa hicho kwa ajili ya kuweka makazi yao na kufanya
biashara zao.
Watu hawa
ndio walio peleka uchawi katika kisiwa cha Ukerewe walio toka nao katika jamii
zao. Inafahamika kuwa wavuvi ni watu wanao jihusisha sana na masuala ya
ushirikina ili waweze kuendelea kufanya shughuli zao za uvuvi bila maruweruwe,
hivyo basi tunapo zungumzia aina ya uchawi hapa, tunazungumzia uchawi mkubwa
kutoka kwenye madhabahu kubwa ya kichawi
No comments:
Post a Comment