Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga,
Simon Msuva, amewapa neno wachezaji wa kikosi hicho akisisitiza kuwa
wana uwezo mkubwa wa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu lakini
wakirekebisha vitu vidogo.
Msuva
ambaye anaichezea Klabu ya Difaa Al Jadida ya nchini Morocco,
aliichezea kwa kiwango timu hiyo ikiwa ni pamoja na kutwaa nafasi ya
ufungaji bora akifungana na Abdulrahman Mussa wa Ruvu Shooting kwa
kufunga mabao 14 kila mmoja.
Yanga ambayo ipo nafasi ya sita ya msimamo wa ligi kwa kuwa na pointi
tisa, imeonekana kuanza kwa kusuasua kwenye ligi ya msimu huu kufuatia
kushinda michezo miwili na kutoa sare mitatu huku wapinzani wao Simba
wakiongoza kutokana na kuwa na pointi 11 hadi sasa, sawa na Mtibwa
Sugar, wakipishana idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.
Msuva
amesema kuwa, kiujumla timu hiyo ni nzuri lakini wanatakiwa
kujitathimini kujua wapi kuna tatizo ili kuweza kutatua kuhakikisha
wanafanikiwa kufanya vyema katika michezo yao inayofuata.
“Yanga wana timu nzuri na kinachotakiwa ni kujua nini wafanye lakini nina imani wanafahamu ili kuweza kupata matokeo mazuri wanatakiwa kufanya nini.
“Wachezaji
wapo vizuri kikubwa wanachotakiwa kukiangalia ni kujiamini kama vile
mwalimu anavyowaamini wao na wasiteteleke na matokeo ya Simba kwani nina
matumaini makubwa kuwa watafanya vyema msimu huu.
“Kikubwa ni pointi tatu ili kuwapa mashabiki kile ambacho wanakihitaji mwisho wa siku kutetea ubingwa,” alisema Msuva.
No comments:
Post a Comment