TIMU ya Tottenham imepata pigo kuelekea mchezo wao wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Manchester UnitedWikiendi hii kufuatia kuumia kwa Harry Kane ambaye anatakiwa kuwa nje kwa maumivu ya nyama za paja.
Spurs
imetoa habari hizo asubuhi ya leo wakiwa kwenye maandalizi ya mwisho
mwisho kuelekea mchezo huo na United wanaoshika nafasi ya pili kwenye
msimamo wa Ligi.
Wamesema kwamba baada ya kufanyiwa vipimo mapema wiki hii, imegundulika ana maumivu ya nyama za paja la mguu wa kushoto.
Kane
aliumia kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Jumapili iliyipita dhidi
ya Liverpool. "Kwa kesho, hatuwezi kufanya kosa kumchezesha,"alisema kocha Mauricio Pochettino kuhusu Kane.
"Ni
maumivu madogo, madogo sana, lakini hatuwezi kufanya kosa. Tutaona
baada ya Jumatano Jumatano dhidi ya Real Madrid. Kesho [Jumamosi]
haiwezekani.
"Ndiyo
[ni pigo], wakati wote unataka wachezaji wote wawepo. Ni tatizo.
Kucheza zaidi au kucheza kidogo, tunataka wawepo wacheze. Wakati wote
tunaamini kwenye umoja, kikosi. Wakati wa msimu, matatizo yanatokea na
lazima uwaamini wachezaji wote, kikosi chote,".
Lakini msimu uliopita, ikiwa bila Kane, Spurs ilicheza mechi saba bila kupoteza, tano ikishinda. Kane amefunga mabao 13 katika mechi 12 za Spurs msimu huu.
Lakini msimu uliopita, ikiwa bila Kane, Spurs ilicheza mechi saba bila kupoteza, tano ikishinda. Kane amefunga mabao 13 katika mechi 12 za Spurs msimu huu.
No comments:
Post a Comment