Sunday, October 22, 2017

Serikali Yatoa Zaidi ya Milioni Mia Sita za Mapambano Dhidi ya Ukimwi

1

Waziri Wa Nchi- Ofisi Ya Waziri Mkuu- (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira Na Watu Wenye Ulemavu Jenista Mhagama (Mb) akizindua rasmi namba ya kuchangia Mfuko wa UKIMWI ambayo ina maana katika mwitikio wa UKIMWI Namba hiyo (0684-90, 90, 90); yaani Asilimia 90 ya watu wanaoishi na VVU wapime afya zao, Asilimia 90 ya waliopimwa na kukutwa na VVU waanzishiwe dawa na Asilimia 90 ya walioanza dawa waweze kufubaza virusi.

 Waziri Wa Nchi-Ofisi Ya Waziri Mkuu- (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira Na Watu Wenye Ulemavu Jenista Mhagama (Mb) ugawaji wa fedha za Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (Aids Trust Fund), ambapo alikabidhi hundi ya  shilingi milioni mia sita na sitini (660,000,000/=) kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kwa ajili ya kununulia dawa za kutibu na kuzuia magojwa nyemelezi kwa Watu waishio na virusi vya Ukimwi



Waziri wa Nchi- Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo(kushoto)  akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Joel Bendera hundi ya kiasi cha milioni mia mbili (200,000,000/=) kwa ajili kusaidia kujenga kituo cha afya Mererani ikiwa ni ahadi ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kusaidia ujenzi wa kituo cha Afya katika eneo hilo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Uratibu Bunge Kazi, Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amekabidhi hundi ya  shilingi milioni mia sita na sitini (660,000,000/=) kwa Waziri wa  Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ajili ya kununulia Cotrimoxazole Tabs / Suspension za watu wanaoishi na VVU.
Akizungumza wakati akikabidhi hundi ya fedha hizo leo Jijini Dar es salaam Waziri Mhagama amesema kuwa dawa hizo ni kwa ajili ya kutibu na kuzuia magojwa nyemelezi kwa wale wanaoishi na virusi vya Ukimwi.(WAVIU).
Akifafanua Mhagama amesema kuwa fedha za wafadhili hazijaelekezwa katika gharama ya ununuzi wa dawa hizo muhimu, hivyo maamuzi ya kununua dawa hizo ni kuziba pengo la gharama za kudhibiti UKIMWI, kama malengo ya Mfuko wa Udhamini wa Kuthibiti UKIMWI (ATF) yalivyo.
Pia, Katika hafla hiyo Waziri Mhagama alikabidhi hundi ya kiasi cha milioni mia mbili (200,000,000/=) kwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara ili kusaidia kujenga kitua cha afya Mererani kwa ajili kusaidia kujenga kituo cha afya Mererani ikiwa ni ahadi ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kusaidia ujenzi wa kituo cha Afya katika eneo hilo.
“Licha ya kuwa Kituo hiki kitasaidia kuboresha afya ya wananchi wote wanaozunguka eneo la Mererani, lakini pia kijatoa huduma kwa Watu waishio na virusi vya Ukimwi na kuwa kitovu cha elimu itakayotolewa kwa makundi mbalimbali ya wananchi katika jitihada za kupunguza maambukizo mapya ya VVU”. Alisema Waziri Mhagama.
Aidha, Mhe. Mhagama aliongeza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wahisani wa ndani pamoja na wananchi wenye nia ya kufanya kazi na serikali katika nyanja mbalimbali ikiwemo udhibiti wa UKIMWI

 

No comments:

Post a Comment