Saturday, October 21, 2017

AFRIKA BARA LETU



MAENEO YAPI YALITUMIKA KUPITISHA DAWA ZA KULEVYA



Kwa mujiblu wa ripoti hii Bara la Afrika liliendelea kutumika kupitisha dawa za kulevya. Afrika Magharibi ilitumika mara kwa mara kupitisha Cocaine na dawa nyingine kuelekea bara la Ulaya wakati Afrika ya Kaskazini iliendelea kuwa chanzo kikuu cha dawa zilizoingia barani Ulaya. Kutumika kwa Afrika ya Mashariki kama kitovu cha kusafirisha heroin iliyotokea Afghanistan ikipelekwa bara la Ulaya kuliongezeka.
Hali hii inachukuliwa kuwa ndiyo sababu ya kuongezeka kwa matumizi ya heroin katika eneo la Afrika ya Mashariki.Wafanyabiashara wa dawa za kulevya waliwalenga watu wenye kipato cha kati ili kuongeza masoko ya dawa hizo katika nchi ambazo biashara hiyo ilipitia zikiwemo za Benini na Namibia.
Ongezeko la biashara ya dawa za kulevya barani Afrika, limeongeza idadi ya watumiaji wa dawa za kulevya hasa vijana wadogo na kuongeza vitendo viovu vinavyofanywa na magenge ya kihalifu. Katika eneo la Afrika ya Magharibi na Afrika ya Kati, uhalifu wa kimtandao ulisababisha madhara makubwa ya kiuchumi na kijamii kwa kukuza biashara ya dawa za kulevya na kuongeza idadi ya wagonjwa wa dawa za kulevya pamoja na kusababisha wahalifu wachache wenye silaha kuhodhi madaraka na mali nyingi.
Ingawa kumekuwepo na jitihada zinazofanywa na nchi za magharibi mwa Afrika kupitia Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi (Economic Community of West Africa-ECOWAS), kwa ujumla, biashara ya dawa za kulevya na matumizi ya dawa hizi katika eneo hili yameongezeka.
Kwa mujibu wa mamlaka zinazosimamia sheria nchini Afrika Kusini, makundi ya kusafirisha dawa za kulevya kutoka China na Eneo la Balkan yalianzishwa katika eneo la kusini mwa Bara la Afrika huku yakijikita katika kusafirisha heroin kupitia Maputo na kuipeleka nchini Afrika Kusini.
 SHERIA, SERA NA HATUA ZILIZOCHUKULIWA NA NCHI ZA AFRIKA
Bara la Afrika limechukua hatua mbalimbali kukabiliana na Tatizo la Dawa za Kulevya. Mwaka 2015 Umoja wa Afrika uliandaa na kujadili Mkakati wa udhibiti wa dawa za kulevya unaojikita zaidi kwenye kuzuia matumizi na kuwatibu watumiaji wa dawa hizo. Aidha, ECOWAS, iliandaa Mpango Kazi wa Kupambana na Biashara ya Dawa za Kulevya na Uhalifu wa Kimataifa katika nchi za Afrika Magharaibi. Nchi za Ghana, Misri na Nigeria ziliimarisha sheria na uwezo wao wa kupambana na dawa za kulevya. Afrika Kusini iliitisha kikao kujadili njia bora zaidi ya kukabiliana na matumizi ya bangi na utegemezi miongoni mwa watumiaji.

No comments:

Post a Comment