Tuesday, October 24, 2017

Wababe wa Tenisi kukutana Dubai

Bingwa mara kumi na mbili wa Grand Slam Novak Djokovic atacheza mechi yake ya kwanza msimu huu kwenye michuano ya tenisi ya Dunia mwezi Desemba huko Abu Dhabi.
 
 
Mcheza tenisi huyo namba saba duniani alipata majeraha ya kiwiko cha mkono mwanzoni mwa msimu huu na kushindwa kuendelea na michuano lakini sasa yupo tayari kurejea kwenye michuano ya tenisi ya Abu Dhabi kuanzia tarehe 28 hadi 30 Desemba.
"Nipo tayari kwa mapambano na wapinzani wangu, nafikiri kitakuwa ni kipimo kizuri kwangu kurejea kwenye ubora”, amesema Djokovic.
Naye mwanafainali wa michuano ya Wazi ya Ufaransa Stan Wawrinka atakuwa anarejea uwanjani baada ya kukaa nje kwa muda mrefu akiuguza maumivu ya goti.

 

Wawrinka raia wa Uswis ambaye anashikilia nafasi ya tisa duniani amekaa nje ya uwanja tangu mwezi Agosti. Michuano ya Abu Dhabi itafanyika wiki mbili kabla ya kuanza kwa michuano ya wazi ya Australia ambayo itakuwa michuano ya kwanza ya Grand Slam ya msimu ujao.
Stan Wawrinka na Novak Djokovic watachuana na wakali wengine akiwemo mchezaji namba moja duniani Rafael Nadal, Dominic Thiem, Pablo Carreno Busta na Milos Raonic.

No comments:

Post a Comment