Wenyeji Azam U-15 wanaongoza ligi hiyo baada ya kuanza kwa kishindo kwa kuifunga Florida 6-0 Jumamosi iliyopita, watakipiga dhidi ya Rendis saa 4.30 asubuhi.
Rendis katika mchezo wake uliopita ilishinda 4-1 dhidi ya New Talent, ambayo imeondolewa kwenye michuano hiyo baada ya kushindwa kuthibitisha umri wa wachezaji wake na nafasi yake kuchukuliwa na Tanzanite ambayo inatokea Temeke, Dar es Salaam.
Florida iliyotoka kupewa kipigo kizito dhidi ya Azam U-15, itashuka tena dimbani kujiuliza pale itakapochuana na Bom Bom ambayo nayo imetoka kupoteza mchezo wa kwanza, zote zikiburuza mkia kwenye ligi hiyo.
No comments:
Post a Comment