Wanachama
wa vyama vikuu viwili vya Union for Democracy pamoja na wa Social
Progress, walikamatwa siku ya Jumapili katika mji wa Lubumbashi, ulioko
Kusini mashariki mwa nchi hiyo, baada ya polisi kuvunja mkutano
waliokuwa nao.
Imeripotiwa kwamba utawala wa Rais,
Joseph Kabila, umepiga marufuku mkutano wa aina yoyote wa kisiasa,
pamoja na maandamano ya upinzani, tangu muda wake wa kukaa madarakani
ka kama Rais kisheria, ulipomalizika mwaka mmoja uliopita.
Hata hivyo imedaiwa kwamba maandamano ya
mara kwa mara ya upinzani nchini humo umekabiliwa vikali na utawala wa
Rais Joseph Kabila.
Kwa upande mwingine chama cha
upinzani, Union for the Congolese Nation, kimesema kwamba, kitajiondoa
katika serikali ya ugawanaji mamlaka, kutokana na kucheleweshwa kwa
uchaguzi mkuu.
Tume ya uchaguzi nchini humo, imesema
kuwa, haitakuwa rahisi kuandaa uchaguzi mkuu wa Urais, kabla ya mwezi
Aprili mwaka ujao wa 2019.
No comments:
Post a Comment